

Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) imefanikiwa kuibuka mshindi wa pili katika tuzo ya Mwezeshaji wa Biashara na Uwekezaji wakati wa Maonesho ya 49 ya Kimataifa ya Biashara yanayoendelea katika Viwanja vya Julius Nyerere jijini Dar es Salaam.
Akizungumza mara baada ya kupokea tuzo hiyo, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa TPA, IJP (Mstaafu) Balozi Ernest Mangu amewapongeza Wafanyakazi wa Mamlaka na kuwataka kutumia ushindi huo kama chachu ya kuendelea kutoa huduma bora zaidi kwa wateja.
Naye Naibu Mkurugenzi Mkuu wa TPA Dkt.Baraka Mdima amewapongeza Wafanyakazi kwa ari kubwa waliyonayo katika kutumikia wateja na kuwataka kuzidisha ari ili kuleta tija zaidi

Naibu Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Hamis Mwinjuma amewataka Watanzania kutumia ushiriki wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) katika Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa kama fursa ya kuuliza na kupata majibu sahihi ya maswali kuhusu shughuli zote za kibandari.
Mhe.Mwinjuma ametoa kauli hiyo Julai 6 2025, alipotembelea banda namba 42 la TPA lililopo Mtaa wa Mataifa katika viwanja vya Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam.

Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC) Nahodha. Mussa Mandia ameipongeza Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) kwa kuendelea kufanya maboresho katika miundombinu ya kuhudumia shehena katika Bandari zote nchini.
Nahodha. Mandia ametoa kauli hiyo Julai 05,2025 alipotembelea banda la TPA katika viwanja vya Maonesho ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba) yanayoendelea jijini Dar es Salaam.

Viongozi wa Menejimenti ya Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) kwa nyakati tofauti wametembelea Banda la TPA katika Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa ( Sabasaba) yanayoendelea katika Viwanja vya Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam.
Viongozi hao ni Mkurugenzi wa Masoko na Uhusiano Dkt. George Fasha na Mkurugenzi wa Bandari ya Dar es Salaam Bw. Abed Gallus Abed, wameeleza kuridhishwa kwao na elimu ya kuhusu shughuli za kibandari inayotolewa bandani hapo na kuwasihi wananchi kujitokeza kwa wingi.
Banda la TPA katika maonesho ya Sabasaba lipo Katika Kitalu namba 42 Mtaa wa Mataifa ambao pia wapo Waendeshaji wa Bandari ya Dar es Salaam, Kampuni za DP World na TEAGTL.
- MV SEA ARIES INAENDELEA KUHUDUMIWA BANDARI YA MTWARA IKIBEBA MITAMBO NA VIFAA VYA MRADI WA UJENZI WA BANDARI YA KISIWA MGAO
- MAMIA WATEMBELE BANDA LA TPA KATIKA MAONEHSO YA SABASABA KUPATA ELIMU KUHUSU SHUGHULI MBALIMBALI ZA KIBNDARI
- KARIBU BANDA LA TPA DAR ES SALAAM INTERNATIONAL TRADE FAIR (DITF), KARIBU TUKUHUDUMIE
- WIZARA YA UCHUKUZI NA MENEJIMENTI YA TPA YAPOKEA UJUMBE KUTOKA UMOJA WA ULAYA