Waziri wa Uchukuzi, Prof. Makame Mbarawa, tarehe 23 Februari, 2026 katika Ziara yake ya Kanda ya Ziwa ametembelea Bandari ya Musoma,na kusisitiza kuwa Serikali inakwenda kuikarabati ili kuendelea kufungua fursa za kiuchumi Mkoa wa Mara
Amesema kuwa Serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan inaendelea na ukarabati na maboresho ya Bandari zote za Maziwa Makuu zikiwemo za Ziwa Nyasa, Tanganyika na Ziwa Victoria kwa lengo la kuimarisha uchukuzi kwa njia ya maji nchini na kuongeza mapato ya wananchi na Mikoa husika sambamba na kufungua uchumi wa kikanda
Akizungumza baada ya kutembelea Bandari ya Musoma, Mkoani Mara Waziri Mbarawa amesema Ziwa Victoria upande wa mkoa wa Mara ndiyo eneo pekee linalopakana na Nchi mbili za Uganda na Kenya hivyo kuna umuhimu mkubwa wa kufanya maboresho ya Bandari ya Musoma ili kuufungua Mkoa wa Mara na kuiufungua nchi Kikanda
Ameeleza kuwa Serikali imeendelea kuwekeza katika miundombinu ya Bandari, ujenzi na ukarabati wa Meli ili kuimarisha usafiri kwa njia ya maji katika Maziwa yote nchini kwa lengo la kuinganisha Tanzania na nchi jirani.
Akizungumza kwa niaba ya Mkoa, Mkuu wa Mkoa wa Mara, Mhe. Kanali Alfredi Mtambi, amesema Bandari ya Musoma ni ya kimkakati, ambapo maboresho yake yataufanya mji wa Musoma kuwa kitovu kikubwa cha biashara, uvuvi na utalii kikanda
Kwa upande wake, Mbunge wa Musoma Mjini, Mhe. Mgore Miraji, ameishukuru Serikali kwa kuendelea kuwekeza katika miundombinu ya usafiri wa majini nchini , akibainisha kuwa maboresho yatakayofanyika kwenye Bandari ya Musoma, wananchi wake na wale wa maeneo ya jirani watanufaika moja kwa moja kupitia ongezeko la shughuli za kiuchumi na fursa za ajira
Ziara hiyo ya Waziri wa Uchukuzi ni sehemu ya mkakati wa Serikali wa kuimarisha Sekta ya Uchukuzi kwa kuboresha Bandari za ndani ya Maziwa Makuu ili kuongeza ufanisi wa usafirishaji na kuchochea maendeleo ya kiuchumi katika Maziwa yote makuu nchin

i
Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) imeishukuru Serikali kwa kuijumuisha miongoni mwa taasisi za umma zilizobahatika kupata waajiriwa wapya ndani ya siku 100 za uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, hatua inayolenga kuimarisha ari, ufanisi na utoaji huduma katika TPA pamoja na Bandari ya Dar es Salaam.
Shukrani hizo zimetolewa , tarehe 23 Februari 2026, na Kaimu Mkurugenzi wa Bandari ya Dar es Salaam, Bw. Abed Gallus Abed, wakati akifungua mafunzo elekezi ya siku moja kwa waajiriwa wapya 95 watakaohudumu katika Bandari ya Dar es Salaam. Mafunzo hayo yamefanyika katika Ukumbi wa Zimamoto na Usalama, Bandari ya Dar es Salaam.
Akizungumza katika hafla hiyo, Bw. Abed amesema kuwa ahadi ya Mhe. Rais ya kuunda ajira mpya ndani ya siku 100 imezaa matunda, ambapo TPA, hususan Bandari ya Dar es Salaam, imepata fursa ya kuongeza watumishi watakaosaidia kuongeza ufanisi na tija katika utendaji kazi.
Aidha, amewataka waajiriwa hao kufanya kazi kwa weledi, nidhamu na kujituma, wakitambua kuwa wanachangia moja kwa moja katika kuchochea ukuaji wa uchumi wa taifa pamoja na nchi jirani zinazotegemea huduma za bandari hiyo.
Pia amewapongeza kwa kuaminiwa na kuajiriwa na TPA, akiwahimiza kuwa chachu ya kuwezesha na kufanikisha biashara kupitia lango kuu la biashara la taifa, kwa kuishi na kutenda kama watumishi waliodhamiria kufungua na kukuza uchumi wa nchi.
Mafunzo hayo elekezi yameenda sambamba na mapokezi rasmi ya watumishi hao wapya, watakaopangiwa katika idara na vitengo mbalimbali vya Bandari ya Dar es Salaam kwa lengo la kuimarisha utoaji huduma na kuongeza ufanisi katika utendaji kazi

.
Naibu Waziri wa Uchukuzi, Mhe. David Kihenzile (Mb), amesema ameridhishwa na maendeleo ya utekelezaji wa miradi ya kimkakati ya inayoendelea mkoani Kigoma, akibainisha kuwa uwekezaji huo una lengo la kuufungua mkoa huo kiuchumi na kuimarisha usafirishaji katika Ukanda wa Maziwa Makuu.
Akizungumza Februari 19, 2026 baada ya kukagua miradi katika Bandari ya Kigoma na Kibirizi, Mhe. Kihenzile amesema Serikali ya Awamu ya Sita inaendelea kuboresha
miundombinu ya bandari ili kuongeza ufanisi wa huduma na mchango wa sekta ya uchukuzi katika uchumi wa Taifa.
Katika Bandari ya Kigoma, mradi unahusisha ujenzi wa gati la abiria, lenye urefu wa mita 130 na upana wa mita 50, barabara ya sakafu ngumu yenye urefu wa takribani mita 500 inayoingia na kutoka bandarini, pamoja na Jengo la Abiria lenye uwezo wa kuhudumia abiria 200 hadi 250 kwa wakati mmoja. Mradi huo unafadhiliwa kwa ruzuku (grant) kutoka Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Japani (JICA) kwa thamani ya dola za marekani milioni 16.9, na hadi sasa umefikia asilimia 9 ya utekelezaji wake ambapo kukamilika kwake kunatarajiwa kurahisisha usafirishaji wa abiria na mizigo, kuongeza ushindani wa bandari na kuimarisha biashara ya kikanda.
Mhe. Kihenzile pia amekagua mradi wa maboresho makubwa ya sehemu ya mizigo katika Bandari ya Kigoma, mradi ambao upo katika hatua za awali za makabidhiano ya eneo la utekelezaji ukilenga kuongeza uwezo wa kuhudumia mizigo, kuimarisha mapato ya Serikali kupitia tozo na kodi, pamoja na kufungua fursa za ajira kwa wananchi wa Kigoma na maeneo jirani. Utekelezaji wake utawezesha mwekezaji kupitisha madini kupitia Bandari ya Kigoma badala ya kutumia njia ya Lobito nchini Angola.
Pia katika kuimarisha maendeleo ya jamii inayozunguka bandari kama sehemu ya utekelezaji wa mpango wa Uwajibikaji kwa Jamii ( CSR), TPA inatekeleza mradi wa usanifu na ujenzi wa Soko la Kisasa la Kibirizi pamoja na Kituo kipya cha Polisi kwa gharama ya Shilingi bilioni 6.4. Soko hilo la kisasa litakuwa na vibanda 250 na uwezo wa kuhudumia wafanyabiashara zaidi ya 500 kwa wakati mmoja.


Naibu Waziri wa Uchukuzi, Mhe. David Kihenzile (Mb), amesema ameridhishwa na maendeleo ya utekelezaji wa miradi ya kimkakati ya inayoendelea mkoani Kigoma, akibainisha kuwa uwekezaji huo una lengo la kuufungua mkoa huo kiuchumi na kuimarisha usafirishaji katika Ukanda wa Maziwa Makuu.
Akizungumza Februari 19, 2026 baada ya kukagua miradi katika Bandari ya Kigoma na Kibirizi, Mhe. Kihenzile amesema Serikali ya Awamu ya Sita inaendelea kuboresha miundombinu ya bandari ili kuongeza ufanisi wa huduma na mchango wa sekta ya uchukuzi katika uchumi wa Taifa.
Katika Bandari ya Kigoma, mradi unahusisha ujenzi wa gati la abiria, lenye urefu wa mita 130 na upana wa mita 50, barabara ya sakafu ngumu yenye urefu wa takribani mita 500 inayoingia na kutoka bandarini, pamoja na Jengo la Abiria lenye uwezo wa kuhudumia abiria 200 hadi 250 kwa wakati mmoja. Mradi huo unafadhiliwa kwa ruzuku (grant) kutoka Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Japani (JICA) kwa thamani ya dola za marekani milioni 16.9, na hadi sasa umefikia asilimia 9 ya utekelezaji wake ambapo kukamilika kwake kunatarajiwa kurahisisha usafirishaji wa abiria na mizigo, kuongeza ushindani wa bandari na kuimarisha biashara ya kikanda.
Mhe. Kihenzile pia amekagua mradi wa maboresho makubwa ya sehemu ya mizigo katika Bandari ya Kigoma, mradi ambao upo katika hatua za awali za makabidhiano ya eneo la utekelezaji ukilenga kuongeza uwezo wa kuhudumia mizigo, kuimarisha mapato ya Serikali kupitia tozo na kodi, pamoja na kufungua fursa za ajira kwa wananchi wa Kigoma na maeneo jirani. Utekelezaji wake utawezesha mwekezaji kupitisha madini kupitia Bandari ya Kigoma badala ya kutumia njia ya Lobito nchini Angola.
Pia katika kuimarisha maendeleo ya jamii inayozunguka bandari kama sehemu ya utekelezaji wa mpango wa Uwajibikaji kwa Jamii ( CSR), TPA inatekeleza mradi wa usanifu na ujenzi wa Soko la Kisasa la Kibirizi pamoja na Kituo kipya cha Polisi kwa gharama ya Shilingi bilioni 6.4. Soko hilo la kisasa litakuwa na vibanda 250 na uwezo wa kuhudumia wafanyabiashara zaidi ya 500 kwa wakati mmoja.


Bandari ya Tanga imetoa rai kwa Watumishi wapya walioripoti kituoni hapo kufanyakazi kwa bidii na kuzingatia sheria na kanuni za utumishi wa umma ili kuhakikisha wanatoa huduma bora yenye tija wakati wote.
Rai hiyo imetolewa na Kaimu Meneja wa Bandari ya Tanga, Bw. Peter Millanzi alipokuwa akiongea na watumishi hao alipokuwa anawakaribisha rasmi.
Bw. Millanzi aliwapongeza watumishi hao na kuwataka kutumia vizuri taaluma waliyonayo katika kutimiza vyema majukumu yao kwa weledi na ufanisi sambamba na kutii sheria na kanuni za utumishi wa umma.
“Kazi za bandari zinatuunganisha na wateja, na ni wajibu wetu kuhakikisha tunawahudumia kwa ukarimu na upendo huku tukifuata miongozo iliyowekwa kwa mujibu wa sheria za utumishi wa umma”. Aliongeza Bw. Millanzi.
Awali akitoa salamu kwa Watumishi hao Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyakazi wa Shughuli za Meli na Bandari (DOWUTA) tawi la Tanga, Bw. Aliko Mwakipagala aliwapongeza watumishi hao na kuwasihi kutojihusisha na tabia zozote zitakazoiletea taasisi taswira mbaya kama vile rushwa, udokozi, utoro na kuchelewa kazini, ulevi na uzembe eneo la kazi.
Bandari ya Tanga imepokea watumishi wapya 33 wenye taaluma nyanja mbalimbali ikiwa ni mpango mkakati wa serikali katika kutimizia ahadi zake kwa watanzania katika utoaji wa ajira nchini

EN
SW
FR
TPA ChatBot - "Nahodha"