

Na Mwandishi Wetu
Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), imeibuka kidedea baada ya kufanikiwa kunyakuwa Ubingwa wa Jumla wa Mashindano ya SHIMMUTA kwa mwaka 2024 katika michuano iliyofanyika jijini Tanga.
Katika mashindano hayo ambayo yalifungwa rasmi na Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, Mhe. Stanslaus Nyongo, yalishuhudia timu nne za TPA zikitawazwa mabingwa rasmi wa mashindano hayo.
Timu ya kwanza kutwaa ubingwa wa mashindano hayo, ni timu ya mpira wa kikapu ya TPA ambayo iliichabanga timu ya NSSF kwa jumla ya vikapu 57 - 45 katika mchezo wake wa fainali. Ubingwa huo ni wan ne mfululizo kwa kwa timu hiyo ya TPA.
Katika mchezo wa mpira wa pete “Netball” timu ya TPA ilitwaa ubingwa huo kwa kuifunga timu ya TMDA kwa magoli 53 – 43 katika mchezo wa fainali ya mashindano hayo. Huo ukiwa ni ushindi wanne mfululizo kwa timu hiyo ya TPA kutawazwa mabingwa wa mashindano hayo kwa mchezo huo.
Kwa upande wa mchezo wa kuvutana kwa Kamba, timu ya wanawake na wanaume zote za TPA, zilishinda michezo yao ya fainali, ambapo timu ya wanawake iliikung’uta timu TPDC, huku wanaume wakiigalagaza timu ya TBS kwa kuichapa katika mtanange uliozikutanisha timu hizo. Timu zote mbili za TPA zimetwaa ubingwa huo kwa mara ya tatu mfululizo.
Na kwa upande wa mchezo wa riadha, timu ya TPA ilishinda katika mbio za mita 200 na kujinyakulia medali za dhahabu, huku katika mikimbio ya wazee ya mita 100, timu ya TPA iliibuka kidedea kwa kupata ushindi wa pili na kujinyakulia medali ya fedha.
Katika michezo ya jadi, timu ya TPA haikuondoka mikono mitupu kwani mwanamama Celine Simon alionyesha umahili wake kwa kuibika mshindi wa tatu katika mchezo huo wa.kusogeza kete yaani 'draft'.
Kufuatia ubingwa huo wa timu zake, TPA imeibuka mshindi wa jumla kwa mara ya pili mfululizo. Mara ya kwanza kuwa mshindi wa jumla ni mashindano ya mwaka 2023 yaliyofanyika mjini Dodoma. Katika mashindano yaliyofanyika mjini tanga mwaka 2024, jumla ya timu 96 kutoka taasisi za umma na binfasi zilishiriki.

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), Bw. Plasduce Mkeli Mbossa, tarehe 26 Novemba 2024, amekutana na kufanya mazungumzo na ujumbe wa Jumuiya ya Wafanyabiashara ya Ubelgiji, Wawekezaji, na Wafanyakazi wa Bandari ya Antwerp.
Ujumbe huo umeongozwa na Balozi wa Ubelgiji nchini Tanzania, Mhe. Peter Huyghebaert, pamoja na Balozi wa Tanzania katika Ufalme wa Ubelgiji na Jumuiya ya Ulaya, Mhe. Jestas Abuok Nyamanga ambapo umetembelea Makao Makuu ya TPA katika Jengo la One Stop Centre, Jijini Dar es Salaam, na kukutana na Menejimenti ya TPA.
Katika mazungumzo yao, waligusia ushirikiano kati ya TPA na Bandari ya Antwerp ya Ubelgiji katika maboresho ya huduma za kibandari, kulingana na mkataba wa ushirikiano uliopo kati ya TPA na Bandari hiyo. Mazungumzo hayo yalilenga kutoa ushauri elekezi wa kufanikisha mabadiliko chanya ya huduma za kibandari nchini pamoja na kuimarisha ushirikiano wa karibu na jumuiya hiyo.
Aidha, mazungumzo hayo yaligusia nia njema ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika maboresho ya Bandari nchini ambapo Bw. Mbossa aliuelezea ujumbe huo kuhusu fursa zilizopo za uwekezaji katika Bandari zote nchini.

TPA Director General, Mr. Plasduce Mbossa attends guests at the reception area of the TPA One Stop Centre building, the headquarter of TPA during the launch of TPA Customer Care Week in Dar es Salaam.

Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) imesema imekuwa ikitekeleza miradi ya kimkakati ili kuvutia shehena ya masoko ya nchi za jirani.
Kauli hiyo imetolewa Desemba 04 2024 na Mkurugenzi wa Masoko na Uhusiano wa TPA Dkt. George Fasha wakati akitoa mada katika Mkutano wa Tano wa Juma la Shughuli za Kibandari na Forodha unaofanyika Jijini Dar es Salaam.
Dkt.Fasha amesema Bandari za Ziwa Victoria zimejengwa kimkakati ili kuvutia shehena inayoenda na kutoka nchini Uganda kutokana na ukaribu wa Kijiografia.
Aidha amesema Bandari za Ziwa Nyasa zimejengwa ili kuvutia soko la Malawi na Zambia wakati Bandari za Ziwa Tanganyika ziko kimkakati kwa ajili ya soko la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
Mbali na hiyo Dkt.Fasha amesema ili kujiweka karibu na Wateja wake TPA imefungua Ofisi katika nchi zote hizo zinazohudumiwa na Bandari za Tanzania.

By Leonard Magomba
Dar es Salaam Port which is Country’s Principal port says is now ready to handle ship as big as to over 305 meters. According to public notice from the Directorate of Marketing and Public Relations of the Tanzania Ports Authority (TPA), the port’s entrance channel has been dredged to the depth of 15.5 meters chat datum with an average channel width of 200 meters. It further says the turning basin has been widened to a diameter of 520 meters with a water depth of 15.5 meters chat datum.
The harbour basin and berths 1-7 have been dredged to 14.5 meters chat datum, while berths 8-11 and the RoRo berth have been dredged to 12.5 meters chat datum. By this modernization means that, the principal port of Dar es Salaam is now ready to handle vessels with a LOA of 305 meters a beam of 40 meters and a draft of 14.5 meters without any tide restrictions.
While under restricted tidal conditions, the port can handle vessels with a LOA of 294 meters, a beam of 32 meters and a draft of 13.5 meters at berths 1-7. Dar es Salaam port is the Tanzania principal port with a rated capacity of over 18 million metric tonnes dry cargo and 6.0 million metric tonnes bulk liquid cargo. The Port has a total quay length of about 2,600 metres with twelve deep-water berths including the RoRo berth. The port handles about 95 percent of the Tanzania international trade.
It serves the land-linked countries of Zambia, Democratic Republic of Congo, Burundi, Rwanda, Malawi, Uganda and Zimbabwe.