

Meli ya MV AFRICAN DIPPER yenye urefu wa mita 179.9, tarehe 10 Machi,2025, imewasili katika Bandari ya Mtwara ikitokea nchini Uturuki ikiwa na shehena ya Sulphur, tani 9,202.54 ( Elfu tisa mia mbili na mbili nukta tano nne)
Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mtwara na Mkuu wa Wilaya ya Tandahimba Mhe. Kanali Michael Mtenjele ameongoza mapokezi ya meli hiyo kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mhe. Kanali Patrick Kenan Sawala ambapo ametoa wito kwa Bodi ya Korosho kuhakikisha kuwa Sulphur hiyo inasambazwa kwa wakati kwa wakulima ili kuleta tija katika uzalishaji wa zao la Korosho.
Naye Meneja wa Bandari ya Mtwara Bw. Ferdinand Nyathi amesema Bandari ya Mtwara imejipanga vema kwa rasilimaliwatu ya kutosha, vitendea kazi na mitambo ili kuhudumia shehena mbalimbali ikiwemo Sulphur.

Watumishi Wanawake wa Bandari ya Mtwara wameungana na wanawake wote Duniani katika kuadhimisha siku ya wanawake Duniani ambayo kimkoa yamefanyika katika Viwanja vya Mashujaa vilivyopo Mjini Mtwara.
Maadhimisho hayo yameongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Mtwara Bw. Abdallah Mwaipaya ambaye ametoa wito kwa Wanawake wote kuungana katika kushiriki shughuli za maendeleo.

Katika kuadhimisha siku ya wanawake duniani, wafanyakazi wanawake wa Bandari ya Tanga wametoa msaada wa vifaa mbalimbali wenye thamani ya Tsh 5,419,000 katika kituo cha “Goodwill Children’s Home “kilichopo kata ya Mwahako Wilaya ya Tanga mjini.
Sambamba na kukabidhi msaada huo wanawake hao walijumuika na watoto hao katika futari maalumu iliyoandaliwa na wafanyakazi hao katika viwanja vya Club ya Bandari.
Akizungumza wakati wa kukabidhi vifaa hivyo, Kaimu Meneja wa Bandari ya Tanga Bw. Peter Millanzi, aliwapongeza wanawake hao kwa kufanya matendo ya huruma kwa watoto hao katika mwezi mtukufu wa Ramadhani jambo ambalo ni baraka na faraja kwa wenye uhitaji.
Awali wanawake hao walishiriki kwenye maandamano ya kuadhimisha siku ya wanawake duniani ambapo Wilaya ya Tanga mjini maadhimisho hayo yamefanyika tarehe 5 Machi ,2025 na kauli mbiu ya mwaka 2025 ni “ Wanawake, Wasichana 2025 Tuimarishe Haki , Usawa na Uwezeshaji”

Wafanyakazi Wanawake wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania(TPA) kituo cha Bandari ya Dar es Salaam wameungana na wanawake wote Duniani kuadhimisha siku ya wanawake duniani ambayo kimkoa yamefanyika katika viwanja vya leaders Club vilivyopo Kinondoni jijini Dar es Salaam.
Maadhimisho hayo yameongozwa na Mkuu wa Mkoa Wa Dar es Salaama Mhe. Albert Chalamila yakiwa na kauli mbiu “Wanawake na Wasichana 2025: Tuimarishe Haki, Urawa na Uwezeshaji.

Matukio mbalimbali katika picha wakati Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Uchukuzi Bw. Ludovick Nduhiye, alipotembelea bandari za Mwanza Kaskazini, Kemondo na Bukoba, tarehe 05 na 06 Machi, 2025 kukagua na kujionea utekelezaji wa miradi ya maboresho na upanuzi wa bandari hizo.
Bw. Nduhiye ameipongeza Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania ( TPA) kwa usimamizi makini na ufanisi wa miradi ya upanuzi na uboreshaji wa bandari hizo ambayo ni jitihada za Serikali kupitia Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania ( TPA) katika kuboresha hali ya usafiri na usafirishaji ndani ya Ziwa Viktoria.
- ZIARA YA MAOFISA WAKIJESHI KUTOKA NCHINI NIGERIA KATIKA BANDARI YA DAR ES SALAAM
- TAARIFA KWA UMMA (UFAFANUZI JUU YA TAARIFA ZISIZO SAHIHI ZA MZIGO INAYOPITA BANDARI YA KIGOMA)
- RAIS DKT. SAMIA AWATAKA WAFANYAKAZI WA TPA KUZIDISHA UFANISI NA UADILIFU KATIKA UTENDAJI
- KIKAO CHA BARAZA LA MAJADILIANO (JIC) LA TPA KITUO CHA BANDARI YA DAR ES SALAAM