

Maofisa wa Kikosi Maalum cha Kuzuia na Kupambana na Megendo Zanzibar KMKM wakiongozwa na Mkuu wa Utawala na Fedha Capt. Fadhil R. Mberua leo tarehe 21 Julai 2025 wamefanya ziara ya kimafunzo katika Bandari ya Dar es Salaam kujifunza kuhusu usalama wa Bandari , mawasiliano na namna ilivyojidhatiti katika kukabiliana na magendo katika kuhakikisha eneo la bahari linakuwa salama.
Ugeni huo ulipokelewa na Afisa Mwandamizi wa Ulinzi na Usalama katika Bandari ya Dar es Salaam Bw. Fortunatus Sandaria kwa niaba ya Kaimu Mkurugenzi wa Bandari ya Dar es Salaam Bw. Abed G. Abed.

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Albert Chalamila, amemuagiza Katibu Tawala Mkoa wa Dar es Salaam Bw. Abdul Mhinte kuunda timu ya wataalamu kutoka Sekta za Umma na Binafsi katika Mkoa wa Dar es Salaam ili kutafuta suluhu ya kudumu ya msongamano wa malori na magari mengine katika Jiji la Dar es Salaam.
Mhe. Chalamila ametoa maagizo hayo tarehe 11 Julai, 2025 alipokutana na viongozi waandamizi wa Mkoa wa Dar es Salaam, Wadau wa Sekta za Umma na Binafsi wanaohusika katika sekta ya Uchukuzi na Menejiment ya Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA).
Aidha, Mhe. Chalamila amewataka Wakala wa Barabara za Vijijini na Mjini (TARURA) na Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) kushirikiana na Jeshi la Polisi kuhakikisha wanaondoa malori yote yanayoegeshwa kando ya Barabara, hususan barabara zinazoingia na kutoka Bandarini.

Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) IJP Mstaafu Balozi Ernest Mangu, ametembelea Banda la TPA na kupongeza ushirikiano uliopo kati ya TPA na wawekezaji.
Akiwa kwenye Banda la TPA katika Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa yanayoendelea katika Viwanja vya Julius Nyerere jijini,Dar es salaam , Balozi Mangu amesema TPA imejipanga kuendelea kuimarisha miundombinu ya Bandari ili kuongeza shehena na ufanisi kwa ujumla.
Kwa kushirikiana na wawekezaji kampuni ya DP World na Tanzania East African Gateway Terminal Limited(TEAGTL) ufanisi wa Bandari ya Dar es Salaam umeimarika kwa kiwango kikubwa na sasa bandari hiyo inaweza kuhudumia meli kubwa.
- TPA YAIBUKA MSHINDI WA PILI KATIKA TUZO YA MWEZESHAJI WA BIASHARA NA UWEKEZAJI WAKATI WA MAONESHO YA 49 YA KIMATAIFA YA BIASHARA
- TUNAKUTAKIA HERI YA SIKU YA SIKUKUU YA SABASABA
- NAIBU WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO ATEMBELEA BANDA LA TPA KATIKA MAONESHO YA SABASABA
- MWENYEKITI WA BODI YA WAKURUGENZI TASAC ATEMBELEA BANDA LA TPA KATIKA MAONESHO YA SABASABA