Select your language

Naibu Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Hamis Mwinjuma amewataka Watanzania kutumia ushiriki wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) katika Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa kama fursa ya kuuliza na kupata majibu sahihi ya maswali kuhusu shughuli zote za kibandari.

Mhe.Mwinjuma ametoa kauli hiyo Julai 6 2025, alipotembelea banda namba 42 la TPA lililopo Mtaa wa Mataifa katika viwanja vya Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam.