Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Albert Chalamila ametoa pongezi kwa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) Bw. Plasduce Mbossa na Meneja wa Bandari ya Tanga Bw. Masoud Mrisha kwa utendaji kazi wao uliotukuka hali iliyopelekea kuongezeka kwa ufanisi katika Bandari ya Tanga.
Mhe. Chalamila alitoa pongezi hizo wakati alipotembelea banda la Bandari ya Tanga kwenye Maonesho ya NaneNane Kanda ya Mashariki 2025, yanayofanyika katika Uwanja wa Mwalimu JK Nyerere Mkoani Morogoro.
Akizungumza mara baada ya kupokea taarifa ya utendaji kazi wa bandari hiyo Mhe. Chalamila alisema kuwa, kuongezeka kwa ufanisi katika Bandari ya Tanga ni pamoja na usimamizi mzuri wa Mkurugenzi Mkuu wa (TPA) pamoja na Meneja wa Bandari hiyo.
Mhe. Chalamila aliongeza kuwa, kuongezeka kwa ufanisi katika bandari hiyo umerahisisha usafirishaji wa shehena ya mazao ya kilimo kutoka Mikoa ya Kanda ya Kaskazini na nchi jirani jambo ambalo ni sifa kwa nchi yetu”.
Aidha Mhe. Chalamila alitoa rai kwa wafanyabiashara nchini kuitumia bandari hiyo kusafirisha mizigo yako kwani usafirishaji kwa njia ya maji hauna mzunguko mrefu na ni salama pia.
Kwa upande wake Afisa Masoko wa Bandari ya Tanga Bw. Ridhiwani Mwasanyagi alimhakikishia Mkuu wa Mkoa huyo bandari ya tanga itaendelea kufanyakazi kwa ufanisi ili kuunga mkono juhudi za Serikali katika kuwezesha biashara kufanyika kwa ufanisi.
Bandari ya Tanga imekuwa ikisafirisha shehena mbalimbali za mazao ya kilimo kwa uchache kama Mkonge Chai , Kahawa, Macademia hivyo ushiriki wa Bandari ya Tanga kwenye Maonesho ya Nanenane Kanda ya Mashariki 2025, ni kutoa elimu kwa umma na wafanyabiashara wa mazo ya kilimo.


Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mhe. Kanali Patrick Kenan Sawalla, tarehe 6 Agosti 2025, ametembelea banda la Bandari ya Mtwara katika maonesho ya 12 ya Wakulima, Wafugaji na Wavuvi (Nanenane) yanayoendelea katika viwanja vya Ngongo vilivyopo Mkoani Lindi.
Mhe. Sawalla amevutiwa na utaratibu unaotumika kutoa elimu ya masuala ya Bandari kwa wadau mbalimbali wanaotembelea banda hilo. Vilevile, amesisitiza kuendelea kujiweka tayari katika kuhudumia shehena ya korosho katika msimu wa mwaka 2025/26.


Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Namibia (NAMPORT) ambao upo Nchini kwa ziara ya mafunzo ya siku mbili, ukiwa na lengo la kujifunza kuhusu Shughuli za utekelezaji Bandarini na utendaji wa kimajukumu wa TPA.
Ujumbe huo wa Maafisa 13 kutoka NAMPORT, umeongozwa na Afisa Rasilimali Watu Mkuu Bi. Johana Hatutale na umepokelewa na Mkurugenzi wa Masoko na Uhusiano wa TPA Dkt. George Fasha kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu Bw. Plasduce Mbossa.
Maafisa hao pia wamepata fursa ya kujifunza kuhusu usimamizi wa rasilimali watu, uboreshaji wa miundombinu ya Bandari na mbinu bora za utoaji huduma kwa wateja na pia utatembelea Chuo cha Bandari (Bandari College) kwa ajili ya kuona namna Tanzania inavyowekeza katika maendeleo ya rasilimali watu kwa ajili ya sekta ya bandari.
Ziara hii ni sehemu ya ushirikiano wa kimataifa wa TPA katika kubadilishana uzoefu, kukuza ufanisi na kuendeleza diplomasia ya bandari Barani Afrika.



Waziri Mkuu Mstaafu Mhe. Mizengo Kayanza Pinda amewaasa wafanyabiashara wa mazao ya kilimo nchini kutumia Bandari ya Tanga kusafirsha mazao yao kwenda kwenye Soko la Kimataifa.
Mhe. Pinda aliyasema hayo alipokuwa mgeni rasmi katika ufunguzi wa Maonesho ya Nanenane Kanda ya Mashariki 2025, yanayojumuisha Mikoa minne ya Tanga, Dar es Salama, Pwani na Morogoro yanayofanyika katika Uwanja wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere maarufu kama “Viwanja vya NaneNane”.
“Bandari ya Tanga inatupa heshima sana katika nchi yetu hivyo natoa rai kwa wafanyabiashara wa mazao ya kilimo nchini kutumia Bandari hiyo ambayo imeboresha huduma zake” aliongeza Mhe Pinda.
Aidha Mhe. Pinda alitoa wito kwa Shirika la Reli la Tanzania (TRC ) na Bandari ya Tanga kuendelea kushirikiana ili kupanua wigo katika utoaji wa huduma katika sekta ya usafirishaji kanda ya mashariki.
Maonesho ya NaneNane Kanda ya Mashariki, kwa mwaka 2025 yanashirikisha Taasisi za umma na binafsi na Bandari ya Tanga ni mshiriki wa maonesho hayo ambayo yenye kauli mbiu ya “Chagua Viongozi Bora kwa Maendeleo Endelevu ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi 2025”.


Mkurugenzi wa Mamlaka ya Hali ya Hewa (TMA) Dkt.Ladislaus Chang’a ameipongeza Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) kwa ufanisi na uweledi katika kuhudumia Shehena.
Dkt.Chang’a ametoa kauli hiyo Agosti 04,2025 alipotembelea banda la TPA lililopo katika Viwanja vya Nzuguni Dodoma yanakofanyika Maonesho ya Wakulima (Nanenane)
Banda la TPA limekuwa kivutio katika Maonesho hayo yanayotarajiwa kufikia kilele Agosti 08, 2025 kwa watu wa rika tofauti kutembelea kwa ajili ya kupata ufafanuzi wa masuala mbalimbali yahusuyo sekta ya Uchukuzi.

- MHE. RAIS DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AZINDUA BANDARI KAVU YA KWALA
- TPA YA SAINI MAKUBALIANO YA TARATIBU ZA UENDESHAJI WA KAWAIDA (SOP's) KWA AJILI YA UHAMISHAJI WA SHEHENA HADI KWALA
- TIMU ZA MPIRA WA WAVU YA TPA ZIMESHIRIKI UFUNGUZI WA LIGI YA MPIRA WA WAVU TAIFA (TVNL)
- WAZIRI WA UCHUKUZI AZUMGUMZA NA WAANDISHI WA HABARI MAKAO MAKUU YA TPA KUHUSU UZINDUZI WA BANDARI KAVU YA KWALA
EN
SW
FR
TPA ChatBot - "Nahodha"