WAIRI MKUU MSTAAFU AWASII WAFANYABIASHARA WA MAZAO KUTUMIA BANDARI YA TANGA NANE NANE

Waziri Mkuu Mstaafu Mhe. Mizengo Kayanza Pinda amewaasa wafanyabiashara wa mazao ya kilimo nchini kutumia Bandari ya Tanga kusafirsha mazao yao kwenda kwenye Soko la Kimataifa.
Mhe. Pinda aliyasema hayo alipokuwa mgeni rasmi katika ufunguzi wa Maonesho ya Nanenane Kanda ya Mashariki 2025, yanayojumuisha Mikoa minne ya Tanga, Dar es Salama, Pwani na Morogoro yanayofanyika katika Uwanja wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere maarufu kama “Viwanja vya NaneNane”.
“Bandari ya Tanga inatupa heshima sana katika nchi yetu hivyo natoa rai kwa wafanyabiashara wa mazao ya kilimo nchini kutumia Bandari hiyo ambayo imeboresha huduma zake” aliongeza Mhe Pinda.
Aidha Mhe. Pinda alitoa wito kwa Shirika la Reli la Tanzania (TRC ) na Bandari ya Tanga kuendelea kushirikiana ili kupanua wigo katika utoaji wa huduma katika sekta ya usafirishaji kanda ya mashariki.
Maonesho ya NaneNane Kanda ya Mashariki, kwa mwaka 2025 yanashirikisha Taasisi za umma na binafsi na Bandari ya Tanga ni mshiriki wa maonesho hayo ambayo yenye kauli mbiu ya “Chagua Viongozi Bora kwa Maendeleo Endelevu ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi 2025”.