Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, amezipongeza Taasisi, Mashirika ya Umma ikiwemo Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) na Kampuni ambazo Serikali inamiliki hisa, kwa utendaji makini na kuonyesha kuridhishwa kwake na mwenendo ambao ni matokeo ya utekelezaji wa maelekezo yake kwa Taasisi na Mashirika ya Umma kuongeza tija na ufanisi katika utendaji.

Mhe. Rais ametoa pongezi hizo tarehe 10 Juni, 2025, Ikulu Jijini Dar es Salaam, katika hafla ya kupokea Gawio la Asilimia 15 ya Mapato ghafi ya Taasisi na Mashirika ya Umma kwa mwaka 2025 ambapo TPA imeibuka kinara katika Taasisi zinazotoa gawio la Asilimia 15 ya mapato ghafi kwa kutoa gawio la Shilingi bilioni 181.5 kutoka Shilingi bilioni 153.917 mwaka 2024.
Huu ni mwaka wa tatu mfululizo kwa TPA kuibuka kinara kwa kutoa gawio kwa Serikali, jambo linalotajwa kuchangiwa na ushirikishwaji wa sekta binafsi ikiwemo DP World na Tanzania East Africa Gateway Terminal katika uendeshaji wa shughuli za Bandari.

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya usimamizi wa Bandari Tanzania Bw. Plasduce Mkeli Mbossa anasikitika kutangaza kifo cha RUTH WILFRED MURUVE aliyekuwa Afisa wa Fedha na Uhasibu katika kituo cha Bandari ya Dar es Salaam kilichotokea tarehe 06 Juni 2025 Jijini Dar es Salaam.
Mungu ailaze roho ya marehemu mahala pema peponi Amani.
Viongozi mbalimbali na Wananchi waliotembelea Banda la Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) lililopo katika Viwanja vya Ukumbi wa Jakaya Kikwete Convention Centre Mjini Dodoma, yanakofanyika Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani, wameipongeza TPA kwa ufanisi mkubwa katika kuhudumia shehena kupitia Bandari zake na kutunza Mazingira ya bahari na Maziwa.
Miongoni mwa Viongozi hao ni Waziri wa Maji Mhe.Jumaa Aweso (Mb) Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe.Khamis Hamza Chilo (Mb) Mkuu wa Mkoa wa Njombe Mhe. Anthony Mtaka na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania ( TMA) Dkt. Ladislaus Chang’a.

Naye Katibu Mkuu wa Machifu wa Mkoa wa Ruvuma Chifu Akida Wabu Mussa ametoa pongezi kwa Menejimenti ya TPA kwa Ujenzi wa Bandari ya Mbamba Bay ambao kimsingi utakuza biashara katika mikoa ya kusini mwa Tanzania.
Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani yamefikia kilele chake Juni 05,2025 ambapo Kitaifa yamefanyika katika Kituo cha Mikutano cha Jakaya Kikwete Mjini Dodoma, yakibeba kauli mbiu isemayo “ Mazingira Yetu na Tanzania Ijayo, Tuwajibike Sasa: Dhibiti Matumizi ya Plastiki.”

Ikiwa katika muendelezo wa kuelekea siku ya Maadhimisho ya Mazingira Duniani, Watumishi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) Juni 04,2025, wameungana na wenzao wa Taasisi zingine zilizochini ya Wizara ya Uchukuzi kupanda miti katika Stesheni Kuu ya Samia Suluhu (SGR) Jijini Dodoma


Kuelekea maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani, Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) Juni 03,2025 imeungana na Taasisi nyingine zilizo chini ya Wizara ya Uchukuzi kushiriki katika zoezi la kufanya usafi eneo la Uwanja wa Ndege wa Dodoma pamoja na maeneo yanayozunguka uwanja huo.

Maadhimisho haya ya kuelekea Siku ya Mazingira Duniani ambayo Kitaifa yatafanyika Mkoani Dodoma chini ya kauli mbiu ya “Mazingira yetu na Tanzania ijayo Tuwajibike Sasa,dhibiti matumizi ya Plastiki”yatafikia kilele Juni 05,2025.
TPA ni mdau makini wa utunzaji wa mazingira ya bahari na maziwa katika maeneo yote zilipo Bandari zake.

EN
SW
FR
TPA ChatBot - "Nahodha"