Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi ( Sekta ya Uchukuzi), Mhe. Atupele Mwakibete, ametembelea na kukagua mradi wa kimkakati wa Maboresho ya Bandari ya Tanga ambao umefikia asilimia 98.9 kukamilika. Mhe. Mwakibete ameridhishwa na kasi ya kukamilishwa kwa Mradi huo kwa wakati na kutoa maelekezo ya kuihuisha haraka iwezekanavyo miundombinu ya Reli inayoingia na kutoka Bandarini hapo ili ianze kufanya kazi haraka.