Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) imepongezwa kwa kuweka mikakati ya kuwajengea uwezo Watumishi wanawake ili waweze kufanyakazi na kuleta matokeo chanya kwa Taasisi na Taifa kwa ujumla.
Hayo yamesemwa na Naibu Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT) ,Uthabiti na Usimamizi wa Sekta ya Fedha Bi.Sauda Msemo katika hafla ya maadhimisho ya siku ya Wanawake Duniani iliyoandaliwa na Wanawake watumishi wa TPA na kufanyika katika jengo la Makao Makuu ya TPA jijini Dar es Salaam Machi 15,2025.
Katika salamu zake za ukaribisho Mkurugenzi wa Rasilimali Watu na Utawala Bw.Mbarikiwa Masinga kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa TPA,amewataka Watumishi wanawake kufanyakazi kwa kushirikiana na kupendana bila kuwekeana chuki ili kufikia malengo makubwa ya Taasisi.
Awali akizungumza wakati akiwakaribisha wageni waalikwa katika hafla hiyo, Meneja Rasilimali Watu wa Bandari ya Dar es Salaam Bi.Mwajuma Mkonga amesema walizindua siku ya Wanawake Duniani kwa kupima afya za wafanyakazi na familia zao katika kituo cha afya kilichopo Bandarini na kutoa misaada ya vifaa tiba vyenye thamani ya shilingi milioni 49 na kwamba TPA imekuwa ikifanya hivyo kwa miaka minne mfululizo.
Katika kuadhimisha siku ya Wanawake Duniani Wanawake watumishi wa TPA walitoa misaada ya vifaa tiba katika hospitali za Wilaya ya Kigamboni vyenye thamani ya shilingi milioni 24 na hospitali ya Rufaa ya Temeke vyenye thamani ya shilingi milioni 25.
Pia katika kuadhimisha siku hiyo wameandaa Tuzo za Mabadiliko Chanya,mwanamke aliyebuni kitu kilicholeta mabadiliko na kuleta tija kwenye Taasisi.
Katika kuadhimisha siku ya Wanawake Duniani,Watumishi wanawake wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) wamebuni shindano la kugombea Tuzo ya Mabadiliko chanya, mchakato uliohitimishwa kwenye halfa iliyofanyika katika ukumbi wa jengo la Makao Makuu wa One Stop Centre jijini Dar es Salaam, Machi 15,2025.
Jaji wa Tuzo hizo Bi.Rosemary Ndesamburo alimtangaza Bi.Lucy Kalinga kuwa mshindi wa tuzo hizo zilizoanza kwa mara ya kwanza mwaka huu huku Bi. Farida Ismaili Hamisi alijinyakulia nafasi ya pili na Bi.Salma Kitwana akipata nafasi ya tatu.

Serikali ya Jamhuri ya Ireland imeeleza dhamira yake ya kuendeleza ushirikiano wa kibiashara na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Bandari za Tanzania.
Kauli hiyo imetolewa Machi 14 2025 na Waziri wa Nchi, Mashauri ya Kigeni na Biashara wa nchi hiyo Mhe. Naele Richmond alipokutana na Menejimenti ya Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) jijini Dar es Salaam.
Katika salamu zake za ukaribisho Naibu Mkurugenzi Mkuu wa TPA Dkt. Baraka Mdima amesema, maboresho makubwa yaliyofanyika katika Bandari zote nchini yamechangia kuongeza ufanisi katika uhudumiaji wa shehena.

Kamati ya kudumu ya Bunge ya Miundombinu imesema imeridhishwa na utendaji kazi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) katika Bandari ya Tanga hasa baada ya maboresho makubwa ya miundombinu yaliyofanywa na Serikali Bandarini hapo.
Kauli hiyo ya Kamati imetolewa tarehe 13 Machi,2025 na Mwenyekiti wake Mhe. Moshi Kakoso (Mb) baada ya kumaliza ziara yao ya kutembelea na kukagua miradi ya maboresho na miundombinu ya Sekta ya Uchukuzi katika Mkoa wa Tanga.
“Tunatoa pongezi nyingi kwa Mheshimiwa Rais, Wizara ya Uchukuzi na TPA kwa maboresho makubwa ya miundombinu yaliyofanyika katika Bandari ya Tanga. Bandari sasa ufanisi unaonekana na mapato yameongezeka, hakika tumeridhishwa”. Amesema Mhe. Kakoso.
Mhe. Kakoso pia amesema kamati yake itaendelea kuisaidia TPA ili kutimiza maono ya Mhe. Rais na kufikia malengo yao na Serikali kwa ujumla.
Kwa upande wake Naibu Waziri wa Uchukuzi Mhe. David Kihenzile (Mb) ameishukuru Kamati kwa ziara yao iliyowawezesha kujionea kazi kubwa inayofanywa na Serikali Katika Sekta ya Uchukuzi. Aidha Mhe. Naibu Waziri Kihenzile ameihakikishia Kamati hiyo kuwa maoni, ushauri na maelekezo waliyoyatoa yatafanyiwa kazi ili kuhakikisha Mkoa wa Tanga unafunguka zaidi kiuchumi kupitia maboresho yanayoendelea kufanywa Miundombinu ya Uchukuzi.
Naye Mkurugenzi Mkuu wa TPA Bw.Plasduce Mbossa, amesema kukamilika kwa awamu mbili za maboresho ya Bandari ya Tanga kwa gharama ya shilingi Bilioni 429.1 kumekuwa chachu ya maendeleo na ufunguo kwa ushoroba wa Kaskazini.
“Manufaa mtambuka ya Bandari ya Tanga yatapelekea maeneo yanayozunguka bandari kufunguka kiuchumi hivyo ushirikiano na wadau wote ikiwemo Kamati yako Mheshimiwa Mwenyekiti ni muhimu ili kufikia malengo yaliyokusudiwa”. Amesema Bw. Mbossa.
Pia Bw. Mbossa ameishukuru Kamati ya Kudumu ya Bunge ya miundombinu kwa kuendelea kutoa ushirikiano kwa TPA ili Mamlaka iweze kutekeleza mipango ya kuboresha miundombinu ya Bandari na kuwa chachu ya Maendeleo ya Uchumi wa Taifa. Aidha amesema TPA inathamini ushirikiano inaoupata kutoka Serikalini, Bunge na Wadau wote wa Sekta ya Bandari na itaendelea kusimamia bandari ya Tanga ili iendelee kutoa huduma kwa ufanisi zaidi.


Mhe. Balozi na Mkuu wa Jeshi la Polisi Mstaafu, Ernest Jumbe Mangu kwa kuteuliwa tena kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA)
Katika kuadhimisha siku ya Wanawake Duniani, Wanawake watumishi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania( TPA) ,tarehe 12 Machi 2025, wameshiriki matendo ya huruma kwa kutoa misaada ya vifaa tiba katika hospitali za Wilaya ya Kigamboni na Temeke vyenye jumla ya thamani ya shilingi milioni 49.
Akipokea vifaa tiba hivyo vya aina 15 tofauti, Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni Mhe.Halima Bulembo amesema hii si mara ya kwanza kwa TPA kutoa misaada katika Wilaya hiyo,na kwa kitendo hicho anaishukuru sana Menejimenti ya TPA.
Akizungumza wakati anakabidhi vifaa tiba hivyo.Meneja Rasilimali Watu wa Bandari ya Dar es Salaam Bi.Mwajuma Mkonga, amesema TPA imetoa vifaa tiba vyenye thamani ya shilingi milioni 24 katika hospitali ya Kigamboni na katika hospitali ya Rufaa ya Temeke wametoa vyenye thamani ya shilingi milioni 25.
Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Temeke, Daktari Bingwa wa macho Annamary Rugakiza Stanslaus, ameishukuru TPA hususani Wafanyakazi wanawake kwa msaada wao ambao utaenda kuwasaidia kwa kuokoa maisha ya wakinamama na watoto wachanga.

- TPA IMEKUTANA NA WAFANYABIASHARA KUTOKA NCHINI UHOLANZI
- BANDARI YA MTWARA YA HUDUMIA MELI YA SULPHR MV AFRICAN DIPPER
- BANDARI YA MTWARA YA ADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI KIMKOA KATIKA VIWANJA VYA MASHUJAA
- BANDARI YA TANGA YAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI KWA KUTOA MSAADA KWA KITUO CHA "GOODWILL CHILDREN'S HOME"
EN
SW
FR
TPA ChatBot - "Nahodha"