TPA YASHIRIKI KATIKA WIKI YA USAFIRI ENDELEVU ARDHINI JNICC
Serikali imesema maboresho yaliyofanyika katika Bandari zote nchini yameongeza uwezo kuhudumia meli kubwa nakupunguza muda wa meli kusubiri.
Kauli hiyo imetolewa na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Mwigulu Nchemba wakati akifungua Maadhimisho ya Kwanza ya Wiki ya Usafiri Endelevu Ardhini katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano wa Mwalimu Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam.
Maadhimisho hayo yenye kauli mbiu ya Ubunifu na Nishati Safi yanaenda sambamba na Maonesho yanayofanyika katika Viwanja vya Mnazi Mmoja ambapo banda la TPA limekuwa kivutio kwa Wadau mbalimbali kufika kwa ajili ya kupata elimu ya shughuli za kibandari.
Waziri Mkuu alitoa tuzo kwa Kampuni ya DP World kuonyesha kutambua mchango wake wa udhamini uliofanikisha Maadhimisho hayo.


EN
SW
FR
TPA ChatBot - "Nahodha"