Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya usimamizi wa Bandari Tanzania Bw. Plasduce Mkeli Mbossa anasikitika kutangaza kifo cha RUTH WILFRED MURUVE aliyekuwa Afisa wa Fedha na Uhasibu katika kituo cha Bandari ya Dar es Salaam kilichotokea tarehe 06 Juni 2025 Jijini Dar es Salaam. 

Mungu ailaze roho ya marehemu mahala pema peponi Amani.