MKUU WA WILAYA ARUSHA AFUNGA MKUTANO WA THATHMINI YA UTENDAJI WA SEKTA YA UCHUKUZI
Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) imepongezwa kwa ufanisi wa uhudumiaji wa shehena kwa haraka na ndani ya muda mfupi.
Kauli hiyo imetolewa Disemba 17 2025 na Mkuu wa Wilaya ya Arusha mjini Mhe.Joseph Mkude alipotembelea banda la TPA katika Viwanja vya Kituo cha Kimataifa cha Mikutano Arusha (AICC) akiwa anamwakilisha Waziri wa Uchukuzi Prof. Makame Mbarawa (Mb) katika kufunga Mkutano wa 18 wa tathmini ya utendaji wa sekta ya Uchukuzi ulienda sambamba na maonesho ya taasisi zilizopo chini ya Wizara ya Uchukuzi, Ujenzi na TAMISEMI uliofanyika kwa siku tatu kuanzia Disemba 15 hadi 17,2025.
Sambamba na kufunga Mkutano na Maonesho hayo, Mhe.Mkude alitoa tuzo kwa taasisi mbalimbali zilizopo chini ya Wizara hizo huku TPA ikipewa tuzo ya “heshima ya uongozi wa mfano, maono, kujitolea na utekelezaji wa Mkataba wa utendaji kazi kati ya taasisi na Wizara.
Katika mkutano huo na maonesho, Viongozi wa serikali, taasisi na sekta binafsi walipata fursa ya kutembelea banda la TPA kwa ajili ya kupata maelezo ya kina kuhusu shughuli za kibandari.


EN
SW
FR
TPA ChatBot - "Nahodha"