Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) Bw. Plasduce Mkeli Mbossa, amesema Bandari za Tanzania zina nafasi kubwa ya kuchangia katika mapato ya nchi na kukuza uchumi kutokana na maboresho makubwa ya miundombinu na uendeshaji yanayoendelea kufanyika. 

Bw. Mbossa amebainisha hayo katika kipindi cha TUNATEKELEZA cha TBC1, akitilia mkazo kwamba, sekta binafsi kama DP World na Tanzania East Africa Gateway Terminal Limited (TEAGTL) wameleta mageuzi makubwa ya utendaji na ufanisi katika Bandari ya Dar Es Salaam kinyume na hofu iliyokuwepo awali.