MAOFISA WA KIKOSI MAALUM CHA KUZUIA NA KUPAMBANA NA MAGENDO ZANZIBAR KMKM WAFANYA ZIARA YA KIMAFUNZO BANDARI YA DAR ES SALAAM

Maofisa wa Kikosi Maalum cha Kuzuia na Kupambana na Megendo Zanzibar KMKM wakiongozwa na Mkuu wa Utawala na Fedha Capt. Fadhil R. Mberua leo tarehe 21 Julai 2025 wamefanya ziara ya kimafunzo katika Bandari ya Dar es Salaam kujifunza kuhusu usalama wa Bandari , mawasiliano na namna ilivyojidhatiti katika kukabiliana na magendo katika kuhakikisha eneo la bahari linakuwa salama.
Ugeni huo ulipokelewa na Afisa Mwandamizi wa Ulinzi na Usalama katika Bandari ya Dar es Salaam Bw. Fortunatus Sandaria kwa niaba ya Kaimu Mkurugenzi wa Bandari ya Dar es Salaam Bw. Abed G. Abed.