KAMPUNI YA SOL SOLUTIONS UMEFANYA ZIARA KATIKA BANDARI YA MTWARA
Bandari ya Mtwara imeendelea kupokea Wafanyabiashara mbalimbali wenye nia ya kuitumia Bandari hiyo kupitisha shehena zao, ambapo Novemba 28,2025, Uongozi wa Kampuni ya SOIL SOLUTIONS wakiongozwa na Meneja wa Miradi Bw. Ashok Shetty, umefanya ziara katika Bandari hiyo kwa lengo la kujiridhisha na uwezo wa Bandari katika kuhudumia shehena.
Bw. Ashok ameeleza kuridhishwa na Bandari ya Mtwara ambapo amefafanua kuwa mwezi Januari 2026 wanatarajia kuanza utekelezaji wa mradi mkubwa wa ujenzi wa Kiwanda kikubwa cha Mbolea ya UREA Mkoani Mtwara. Kiwanda hicho kitakuwa na uwezo wa kuzalisha Tani 1,750 kwa siku ambapo asilimia 80 ya uzalishaji huo utasafirishwa kwenda katika masoko mbalimbali ya kimataifa.
Vilevile, ameeleza kuwa wakati wa kuanza kwa mradi wa ujenzi, wanatarajia kuitumia Bandari ya Mtwara kupitishia vifaa vya ujenzi kiasi cha zaidi ya Tani 20,000.
Kaimu Meneja wa Bandari ya Mtwara Bw. Mtunze Sudi ameeleza kuwa Bandari ina uwezo mkubwa na ipo tayari kuhudumia shehena hizo kufuatia uwepo wa miundombinu wezeshi, vitendea kazi vya kisasa na rasilimaliwatu wa kutosha.


EN
SW
FR
TPA ChatBot - "Nahodha"