BANDARI YA TANGA YAFANYA KIKAO CHA BARAZA JIJINI TANGA
Meneja wa Bandari ya Tanga, Bw. Salehe Mbega, ametoa pongezi kwa Menejimenti na Chama cha Wafanyakazi wa Shughuli za Meli na Bandari (DOWUTA) kituo cha Tanga kwa namna wanavyoshirikiana kuhakikisha Bandari ya Tanga inafikia malengo yaliyowekwa.
Bw. Mbega alitoa pongezi hizo alipokuwa anafunga Kikao cha 70 cha Baraza la Majadiliano la kituo hicho kilichofanyika katika Ukumbi wa Mikutano katika Jengo la Bandari (Bandari House).
“ Nawapongeza Menejimenti na Upande wa wawakilishi wa Chama (DOWUTA) kwa namna mnavyoshirikiana na kuwa na lengo moja kuhakikisha bandari yetu inafanyakazi vizuri”.
Alisema Mbega Naye Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyakazi wa Shughuli za Meli na Bandari (DOWUTA), Bw. Aliko Mwakipagala alimuhakikishia Meneja huyo kuendelea kuchapa kazi na kupokea maelekezo mbalimbali yatakayokuwa yanatolewa ili kuongeza tija na ufanisi.
Katika kikao hicho hoja mbalimbali zilijadiliwa na changamoto mbalimbali zilitafutiwa ufumbuzi ili kuhakikisha shughuli za kibandari zinafanyika kwa ufanisi.


EN
SW
FR
TPA ChatBot - "Nahodha"