BANDARI YA TANGA YAENDELEA KUTOA HUDUMA KWA KUPITIA MIFUMO
Katika kuadhimisha Wiki ya Huduma kwa Wateja “Customer Service Week” Bandari ya Tanga Kitengo cha Tehama kimeendelea kutoa huduma bora kwa wateja kupitia mifumo.
Akizungumza juu ya maadhimisho hayo ambayo hufanyika kila mwaka mwezi Oktoba, Afisa Mwandamizi Kitengo cha Tehama Bandari ya Tanga Bw. Johanes Rwezaula alisema kuwa katika kuwezesha utoaji wa huduma bora kwa wateja miundombinu ya mawasiliano katika bandari hiyo yameimarika.
“Miundombinu ya mawasiliano imeboreshwa na mifumo imeimarika hakuna tena changamoto za mara kwa mara za kukatika kwa mtandao jambo ambalo limesaidia kurahisisha utendaji kazi katika utoaji wa mizigo na upatikanaji wa taarifa” Aliongeza Rwezaula.
Aidha pia Rwezaula alisema kuwa mifumo inayotumika bandarini ya ITOS na POAS ambayo imeunganishwa na mifumo ya Taasisi zingine kama Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kama TANCIS na Wizara ya Fedha GePG imesaidia utendaji kazi bandarini, hivyo aliwataka wateja waendelee kufurahia huduma zinazotolewa bandarini hapo.


EN
SW
FR
TPA ChatBot - "Nahodha"