Bandari ya Mtwara imeendelea kupata pongezi kutoka kwa Wadau mbalimbali waliopo kwenye mnyororo wa thamani wa Sekta ya Madini, kufuatia maboresho mbalimbali yaliyofanyika katika miundombinu, mifumo na vitendea kazi ili kuongeza ufanisi na utendaji kazi wa Bandari.

Pongezi hizo zimetolewa katika maonesho ya Madini na Fursa za Uwekezaji Mkoa wa Lindi yaliyofunguliwa rasmi tarehe 11 Juni 2025 na Waziri wa Maji, Nishati na Madini wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Mhe. Shaib Hassan Kaduara.