WANAWAKE MAKAO MAKUU NA BANDARI YA DAR ES SALAAM WASHILIKI MAADHIMISHO SIKU YA MWANAMKE DUNIANI
Wanawake wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) wameungana na wanawake wengine kutoka taasisi mbalimbali kushiriki katika maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani yaliyofanyika katika viwanja vya Mburahati, Wilaya ya Ubungo Jijini Dar es Salaam.
Maadhimisho ya mwaka huu yameongozwa na kaulimbiu isemayo “Haki na Usawa kwa Wanawake na Wasichana: Msingi Jumuishi Kufikia Dira ya Maendeleo 2050.” Kaulimbiu hiyo inalenga kuhimiza jamii kuhakikisha wanawake na wasichana wanapata haki sawa na fursa katika nyanja zote za maendeleo.
Mgeni rasmi katika maadhimisho hayo alikuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mhe. Albert John Chalamila, ambaye alisisitiza umuhimu wa kuendelea kuwawezesha wanawake kiuchumi na kijamii ili waweze kushiriki kikamilifu katika maendeleo ya taifa.
Akizungumza wakati wa maadhimisho hayo, Mhe. Chalamila alieleza kuwa wanawake wana mchango mkubwa katika maendeleo ya nchi, hivyo ni muhimu kuendelea kuondoa vikwazo vinavyowazuia kupata haki na fursa sawa katika elimu, ajira na uongozi.
Wanawake wa TPA walishiriki katika shughuli mbalimbali za maadhimisho hayo ikiwemo maandamano, maonesho na ujumbe wa kuhamasisha jamii kutambua na kuheshimu haki za wanawake na wasichana.
Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani huadhimishwa kila mwaka tarehe 8 Machi, yakilenga kutambua mchango wa wanawake katika maendeleo ya jamii pamoja na kuhimiza usawa wa kijinsia.



EN
SW
FR
TPA ChatBot - "Nahodha"