Select your language

Msafara wa viongozi mbalimbali wanaosoma katika Chuo cha Taifa cha Ulinzi (NDC), Machi 12, 2026 wametembelea Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) kwa ajili ya kujifunza shughuli za kibandari.

 

Wakiongozwa na Mkurugenzi wa Mafunzo wa Chuo hicho, Dkt. Osward Masebu wanafunzi hao ambao ni vingozi wa kada mbalimbali walipata fursa ya kuelezwa kwa kina shughuli za utekelezaji za kibandari na Dkt Boniface Nobeji ambaye alimwakilisha Mkurugenzi Mkuu wa TPA, Bw. Plasduce Mbossa ambaye naye ni miongoni mwa wanafunzi hao.

 

Naye Mkurugenzi wa Mafunzo wa Chuo hicho, Dkt. Osward Masebu amesema kwamba wanaishukuru TPA kwa mapokezi mazuri na kuwapa maelezo ya kina kuhusu shughuli za Mamlaka