Select your language

Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) Dkt. Baraka Mdima ( Wa pili kulia aliyevaa miwani) anahudhuria Mkutano wa Tatu wa Umoja wa Mataifa wa Nchi zisizo na Bahari ( LLDC3) unaofanyika mjini Awaza, Turkmenistan kuanzia Agosti 5 hadi 8 ,2025. 

Mkutano huo unalenga kutathmini utekelezaji wa Mpango wa Maendeleo wa Vienna wa 2014- 2024 na kuweka ajenda mpya ya maendeleo jumuishi kwa miaka kumi ijayo, huku ukijadili changamoto mbalimbali zikiwemo gharama kubwa za usafirishaji, utegemezi wa nchi jirani na miundombinu kwa nchi zisizo na Bahari.