Select your language

Matukio mbalimbali katika picha wakati Mabalozi wapya wanne, walipofanya ziara ya kikazi Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) ili kujifunza shughuli za utekelezaji Bandarini na kufahamishwa masuala muhimu yatakayowasaidia katika nchi wanazokwenda kuiwakilisha Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, tarehe 25 Aprili 2025.

Mabalozi hao ni Mhe. Balozi Dkt. Habibu Kambanga, aliyepangiwa kwenda nchini Rwanda, Mhe. Balozi Dkt. Suzan Kaganda, aliyepangiwa kuhudumu nchini Zimbabwe, Mhe. Balozi Mobhare Matinyi, aliyepangiwa nchini Sweden na Mhe. Balozi Hamad Hamad, aliyepangiwa kwenda nchini Msumbiji na walipokelewa na kupata maelezo ya kina kutoka kwa Kaimu Mkurugenzi wa huduma za Uhandisi Mha. Erick Madinda.