BARAZA LA WAFANYAKAZI TPA MAKAO MAKUU LAFANYA KIKAO CHA 39 BAGAMOYO
Baraza la Wafanyakazi kituo cha Makao Makuu (HQ) limefanya Kikao chake cha thelathini na tisa (39) mjini Bagamoyo Mkoa wa Pwani.
Baraza hilo limelenga kupokea taarifa ya utekelezaji wa malengo kwa mwaka wa fedha 2025/2026 kwa kipindi cha nusu mwaka cha (Julai - Desemba,2025) pamoja na kupokea na kujadili mapendekezo ya Mpango wa Bajeti ya mwaka wa fedha 2026/2027.
Pamoja na mambo mengine Baraza hilo limefanya Uchaguzi wa wajumbe wa kamati ya Utendaji ya Baraza la Uchumi wa tawi la Makao Makuu ambapo washindi katika uchaguzi huo ni Bw. Nassour A. khalifa, Bw. Erick V. Hatia, Bi. Lilian Nicolaus Bhoke na Bi Aziza J. Abdulrahmnan.
Aidha Kati ya hao wawili wameteliwa kuwa Wajumbe wa Baraza kuu la Uchumi la Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania ((TPA) ambao ni Bi. Aziza J. Abdulrahman na Bw. Nassor A. Khalifa.
Baraza hilo limeongozwa na Mkurugenzi wa Huduma za Tehama Bw. Abdulatif A. Minhajj kwa niaba ya Naibu Mkurugenzi Mkuu wa TPA Dkt. Baraka R. Mdima


EN
SW
FR
TPA ChatBot - "Nahodha"