Mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya CRDB, Bw. Charles Carley, ameipongeza Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) kwa juhudi madhubuti za kupanua wigo wa soko katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), hususani kupitia huduma zinazotolewa katika Mkoa wa Lualaba.

Pongezi hizo zimetolewa tarehe 16 Juni 2025, katika ziara rasmi ya ujumbe wa Utawala wa Benki ya CRDB-Congo walipotembelea ofisi ya TPA mkoani Kolwezi, kisha kushiriki mkutano muhimu baina ya TPA, CRDB na Shirikisho la Makampuni ya Biashara Congo (FEC) – Lualaba.

Mkutano huu ni sehemu ya muendelezo wa mashauriano ya kibiashara yaliyoanzishwa kupitia kongamano la wadau lililoandaliwa na TPA mwezi Aprili 2025 chini ya kaulimbiu isemayo “Kwa pamoja tunatengeneza kesho bora si ya TPA na sekta ya biashara ya Lualaba pekee, bali pia mafanikio ya kiuchumi ya Tanzania na DRC kwa ujumla.”

Kwa niaba ya TPA, Afisa Mwakilishi Bi. Kuruthum Ngunguti alieleza umuhimu wa ushirikiano na taasisi za kifedha kama CRDB katika kurahisisha michakato ya malipo ya huduma za bandari, jambo linaloongeza ufanisi na kuimarisha uzoefu wa wateja wa TPA.

Tuwasiliane

Kwa maswali yoyote au msaada, wasiliana nasi muda wote (24/7)
0800-110032
S. L. P 9184 Dar es salaam
dg@ports.go.tz
255 22 2130390

Habari na Matukio DRC

TPA YAPONGEZWA NA MJUMBE WA BODI YA CRDB KWA JUHUDI ZA KUPANUA...

01 Julai 2025

Mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya CRDB, Bw. Charles Carley, ameipongeza Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) kwa juhudi madhubuti za kupanua wigo wa soko katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC),...
  Soma Zaidi
NEWLY APPOINTED TANZANIA CONSUL GENERAL OFFICIAL VISIT TO TPA OFFICE IN LUBUMBASHI...

06 Juni 2025

Busy Day at TPA Lubumbashi Office! On June 5th, 2025, the newly appointed Tanzania Consul General in Lubumbashi, DRC, Hon. Magubilo Muroba, paid an official visit to the Tanzania Ports Authority (TPA) office in Lubumbashi.  Hon. Muroba...
  Soma Zaidi