WAFANYAKAZI WA BANDARI YA MTWARA WAPEWA SEMINA YA ULINZI NA USALAMA BANDARINI
Wafanyakazi wa Bandari ya Mtwara wameshiriki katika semina ya mafunzo ya Ulinzi na Usalama wa Bandari (ISPS Code) yaliyofanyika tarehe 16 Disemba, 2025 Mkoani Mtwara.
Mafunzo hayo yameongozwa na Mkufunzi ambaye ni Afisa Sheria Mwandamizi kutoka Makao Makuu ya Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania Bw. Khalid Kitentya yamelenga kuwajengea uwezo na uelewa wa kina Wafanyakazi kuhusu taratibu, wajibu na mbinu bora za kuimarisha ulinzi na usalama wa Bandari kwa mujibu wa viwango vya Kimataifa vya ISPS Code.
Akifungua rasmi mafunzo hayo kwa niaba ya Meneja wa Bandari ya Mtwara, Afisa Utawala Mwandamizi Bi. Fassie O. Mushi amewahimiza wafanyakazi kushiriki kikamilifu na kuzingatia mafunzo hayo muhimu. Alisisitiza kuwa, matokeo chanya ya mafunzo hayo yatasaidia kuiweka Bandari katika hali ya usalama zaidi.
Mafunzo hayo ni sehemu ya juhudi zinazoendelea za Bandari ya Mtwara katika kuboresha usalama ili kuendana na viwango vya Kimataifa vya uendeshaji wa Bandari.


EN
SW
FR
TPA ChatBot - "Nahodha"