VIONGOZI WATEMBELEA BANDA LA TPA LILILOPO KATIKA UKUMBU WA JAKAYA KIKWETE DODOMA

Viongozi mbalimbali na Wananchi waliotembelea Banda la Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) lililopo katika Viwanja vya Ukumbi wa Jakaya Kikwete Convention Centre Mjini Dodoma, yanakofanyika Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani, wameipongeza TPA kwa ufanisi mkubwa katika kuhudumia shehena kupitia Bandari zake na kutunza Mazingira ya bahari na Maziwa.
Miongoni mwa Viongozi hao ni Waziri wa Maji Mhe.Jumaa Aweso (Mb) Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe.Khamis Hamza Chilo (Mb) Mkuu wa Mkoa wa Njombe Mhe. Anthony Mtaka na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania ( TMA) Dkt. Ladislaus Chang’a.
Naye Katibu Mkuu wa Machifu wa Mkoa wa Ruvuma Chifu Akida Wabu Mussa ametoa pongezi kwa Menejimenti ya TPA kwa Ujenzi wa Bandari ya Mbamba Bay ambao kimsingi utakuza biashara katika mikoa ya kusini mwa Tanzania.
Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani yamefikia kilele chake Juni 05,2025 ambapo Kitaifa yamefanyika katika Kituo cha Mikutano cha Jakaya Kikwete Mjini Dodoma, yakibeba kauli mbiu isemayo “ Mazingira Yetu na Tanzania Ijayo, Tuwajibike Sasa: Dhibiti Matumizi ya Plastiki.”