MKUU WA MKOA MTWARA AFANYA ZIARA KATIKA BANDARI YA MTWARA
Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Mhe. Kanali Patrick Kenan Sawala, ameeleza kuridhishwa kwake na maandalizi makubwa yaliyofanywa na wadau wote wanaohusika katika mnyororo wa thamani wa zao la Korosho.
Mhe. Kanali Sawala ametoa kauli hiyo tarehe 10 Novemba 2025, baada ya kufanya ziara ya kukagua maeneo yatakayotumika kufungashia shehena ya korosho (stuffing areas) pamoja na kutembelea Bandari ya Mtwara.
Amesema ana imani kubwa kuwa korosho zote zinazolimwa mikoa ya Kusini ya Mtwara, Lindi na Ruvuma, zinazokadiriwa kufikia takriban tani 700,000 msimu wa 2025/2026 zitasafirishwa kupitia Bandari ya Mtwara.
Katika ziara hiyo, Mhe. Kanali Sawala aliambatana na Kamati ya Usalama ya Mkoa wa Mtwara, Mkuu wa Wilaya ya Mtwara Mhe. Abdallah Mussa Mwaipaya, Menejimenti ya Bandari ya Mtwara, pamoja na viongozi kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na Bodi ya Korosho Tanzania (CBT).
Kwa upande wake, Meneja wa Bandari ya Mtwara, Bw. Ferdinand Nyathi, alibainisha kuwa bandari imejipanga kikamilifu kutoa huduma bora kwa msimu huu wa usafirishaji wa korosho kwa kuwa na miundombinu imara, vifaa vya kutosha, na rasilimali watu wenye weledi.


EN
SW
FR
TPA ChatBot - "Nahodha"