BODI YA WAKURUGENZI YAFANYA ZIARA KATIKA BANDARI YA UVUVI YA KILWA
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania IGP Mstaafu Mhe. Balozi Ernest J. Mangu ameongoza wajumbe wa Bodi hiyo katika ziara ya kukagua mradi wa ujenzi wa Bandari ya Uvuvi ya Kilwa, tarehe 10 Oktoba 2025.
Ziara hiyo ilihusisha kutembelea miundombinu ya Bandari na kupata taarifa ya utekelezaji wa ujenzi wa Bandari hiyo ya kisasa ambao unatekelezwa na Kampuni ya CHEC ya Nchini China ili kushuhudia hatua na hali halisi ya mradi huo ilivyo kwa sasa.
Mhe. Balozi Mangu alieleza kuridhishwa na kasi ya utekelezaji wa ujenzi wa Bandari hiyo ambayo inatarajiwa kuchakata zaidi ya Tani 60,000 za shehena ya samaki kwa mwaka mara itakapokamilika na kuanza kazi.
Kwa upande wake, Mhandisi wa Kampuni ya CHEC Bw. Douglas Semwenda ameeleza kuwa, mradi huo wenye thamani ya Shilingi Bilioni 266 ulianza kutekelezwa mwezi Septemba, 2023 ambapo kwa sasa umefikia asilimia 88 ya utekelezaji wake na unatarajiwa kukamilika rasmi mwezi Februari, 2026.


EN
SW
FR
TPA ChatBot - "Nahodha"