BANDARI YA TANGA YAADHIMISHA WIKI YA HUDUMA KWA WATEJA
Katika kuhakikisha Kauli Mbiu ya maadhimisho ya Wiki ya Huduma kwa Wateja kwa mwaka 2025 “Mission Possible” inatekelezwa kwa vitendo, Bandari ya Tanga imejipanga kuilinda mizigo ya wateja ili iweze kutoka bandarini ikiwa salama.
Uhakikisho huo umetolewa na Afisa Ulinzi Mwandamizi wa Bandari ya Tanga Bw. Rajani Fidu Hussein katika mwendelezo wa wiki ya Huduma kwa Wateja alipokuwa anawahudumia huduma maeneo katika yake ya kazi.
Bw. Fidu alisema kuwa Bandari ya Tanga ni salama ulinzi wa mizigo ni wa uhakika, hivyo nawashauri wateja waendelee kutumia Bandari ya Tanga ambayo iko tayari kutoa huduma na kutatua changamoto za wateja usiku na mchana.


EN
SW
FR
TPA ChatBot - "Nahodha"