Jumla ya maofisa 44 kutoka Chuo Cha Kijeshi kilichopo Duluti Arumeru Mkoani Arusha wametembelea Bandari ya Tanga kwa lengo la kujifunza na kuona utendaji wa Bandari. Akiongea kwa niaba ya Maafisa hao, Mkuu wa msafara huo, Kanali W. Mwamunyange alibainisha kuwa lengo la ziara hiyo ni kujifunza na kuona shughuli zinazofanywa na Bandari. Amengeza kuwa mbali ya hiyo, ziara hiyo pia inawasaidia kujenga uhusiano mzuri katika ulinzi na usalama kwenye maeneo mbalimbali ya mipaka ya Tanzania. Maafisa hao ni wanafunzi wanaotoka katika nchi za Tanzania, Burundi, Rwanda, Zambia, Zimbabwe, Malawi, Nigeria, Kenya, Misri na India. Sehemu ya maofisa 44 kutoka Chuo Cha Kijeshi kilichopo Duluti Arumeru Mkoani Arusha wametembelea Bandari ya Tanga Baadhi ya maofisa 44 wa kijeshi wakiwa Bandari ya Tanga Maofisa 44 kutoka Chuo Cha Kijeshi kilichopo Duluti Arumeru Mkoani Arusha wakiwa katika picha ya pamoja Mwisho
Waziri wa Uchukuzi Prof.Makame Mbarawa akionyeshwa maendeleo ya ujezi wa mradi wa Lagosa na mwenyeji wake, Naibu Mkurugenzi Mkuu, Mhandisi Juma Kijavara. Serikali kupitia Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) ipo katika hatua za mwisho kukamilisha ujenzi wa Bandari ya Lagosa iliyopo katika Kijiji cha Mgambo Wilayani Uvinza, mkoani Kigoma. Akizungumza mara baada ya kukagua maendeleo ya mradi huo Waziri wa Uchukuzi Prof.Makame Mbarawa amesema ujenzi huo unaogharimu TZS.15 bilioni tayari umefikia asilimia tisini na sita na kusisitiza ifikapo mwezi Aprili mwaka 2024 mradi huo uwe umekamilika, Aidha Prof.Mbarawa amesema uwepo wa bandari hiyo utachagiza ufanisi wa shughuli za kiuchumi hasa Kilimo ,uvuvi na biashara kwa wakazi wa mwambao wa ziwa Tanganyika ambao kupitia bandari hiyo wataweza kusafiri na kusafirisha bidhaa zao kwenda nje ya nchi. Kwa upande wake Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), Mhandisi Juma Kijavara amesema Mamlaka imejipanga kukamilisha ujenzi huo haraka ili bandari hiyo ianze kutoa huduma kwa wananchi. Naye Mkuu wa Wilaya ya Uvinza, Bi. Dina Masamani ameishukuru Serikali kwa kujenga Bandari hiyo akisisitiza kuwa itawezesha wakazi wa eneo hili kufanya shughuli za kiuchumi na kijamii ikiwemo kusafirisha bidhaa kwenda Nchi jirani ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo ambayo ipo umbali wa takribani 88km kutoka ilipo Bandari ya Lagosa. Waziri akikagua mradi Waziri akikagua mradi na wenyeji wake Muonekano wa Gati la Bandari ya Lagosa Muonekano wa Gati la Bandari ya Lagosa
Kampuni ya China Harbour Engineering leo imekabidhi kwa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) mradi mkubwa wa kimkakati wa maboresho ya Bandari ya Tanga baada ya kazi kubwa ya utekelezaji wa mradi huo. Mradi huo ulihusisha uongezaji kina wa mlango wa bandari (entrance channel) kutoka mita 3 mpaka mita 13, sehemu ya kugeuzia meli (turning basin) na uongezaji wa kina cha gati kutoka mita 3 mpaka mita 13. Lengo la mradi huo ni kuhakikisha Bandari ya Tanga inahudumia meli kubwa na gatini na shehena kubwa ya mzigo kutoka tani 750,000 za sasa mpaka tani milioni tatu kwa mwaka. Akipokea mradi huo, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TPA, Mhandisi Juma Kivajara ameishukuru Serikali kwa uwekezaji mkubwa na Kampuni ya CHEC kwa utekelezaji wa mradi huo kwa ufanisi na kiwango bora. Akiongea katika makabidhiano hayo, Eng. Kijavara amewataka wafanyakazi wa Bandari ya Tanga kufanya kazi kwa bidii ili kuongeza kiasi cha shehena ya mzigo kulingana na malengo yaliyowekwa na Mamlaka. Aidha Eng. Kijavara amesema TPA itaendelea kuboresha Bandari ya Tanga kwa kujenga gati mpya ya urefu wa mita 250, gati ya meli za abiria yenye urefu wa mita 50 pamoja na ujenzi wa "One Stop Center". Mwisho
Mhandisi Juma Kijavara akifungua mkutano huo Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) imejipanga kuhudumia Shehena ya zao la Korosho kupitia Bandari ya Mtwara. Mkakati huo uliobainishwa na Mkurugenzi Mkuu wa TPA, Bw. Pasduce Mbossa, ni sehemu ya utekelezaji wa maagizo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan. Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wakati wa Mkutano wa Wadau wa Bandari kuhusu maandalizi ya usafirishaji wa zao la Korosho kupitia Bandari ya Mtwara, Naibu Mkurugenzi Mkuu, Mhandisi Juma Kijavara amesema Bandari ya Mtwara ipo tayari kuhudumia shehena hiyo. “Sisi kama TPA tumejipanga vizuri kabisa kuhudumia Shehena hiyo ikiwa ni utekelezaji wa maagizo ya Mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kuhusu matumizi ya Bandari ya Mtwara kusafirisha zao la Korosho. Kama sehemu ya utekelezaji wa maelezo hayo, tayari TPA imepenga kuongeza vitendea kazi kama Kreni mbili zenye uwezo wa kubeba tani 160 za mzigo kila moja ili kuongeza ufanisi wa huduma katika usafirishaji wa zao la Korosho katika Bandari ya Mtwara. Wadau wakiwa kwenye kikao hicho Wadau wakiwa kwenye kikao hicho washiriki wa mkutano huo
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amefurahishwa na ufanisi wa kiutendaji katika Bandari ya Mtwara hasa baada ya maboresho makubwa kufanyika katika Bandari hiyo. Akizungumza na Watumishi wa Bandari ya Mtwara baada ya kukagua maendeleo ya Mradi wa Maboresho wa Bandari hiyo, Rais Dkt. Samia amesema Maboresho makubwa yaliyofanyika Bandarini hapo yameongeza ufanisi na kuufungua kiuchumi Mkoa wa Mtwara na Mikoa ya Kusini mwa Tanzania. “Serikali yangu itaendelea kuongeza Bajeti ya kuboresha miundombinu ya Bandari ili kuvutia zaidi wateja, wadau wafanyabiashara wa usafirishaji bidhaa mbalimbali ili kuongeza ushawishi wa kuzitumia zaidi Bandari zetu,” amesema Rais Dkt. Samia. Vilevile, Rais Dkt. Samia amesema Serikali yake imejiandaa kusafirisha Korosho kupitia Bandari ya Mtwara, hivyo ametoa wito kwa Wananchi kujiandaa kuiunga mkono Serikali kwa kuongeza mapato yatokanayo na shughuli za Bandari. Rais Dkt. Samia pia ametoa rai kwa watumishi wa Bandari ya Mtwara kufanya kazi kwa bidii na weledi mkubwa ili Bandari hiyo ifikie kiwango cha Bandari ya Dar es Salaam. Miradi iliyotekelezwa ni sehemu ya maboresho ya utendaji kazi wa Bandari ya Mtwara ni pamoja na ujenzi wa Gati namba 2 lenye urefu wa mita 300, ujenzi wa mita ya kupakua na kupimia mafuta ili kuhakikisha mafuta yanayoshushwa katika Bandari ya Mtwara yana ubora stahiki Pamoja na ujenzi wa sehemu ya kuhifadhi makasha na ukarabati wa ghala na vifaa vya kuhudumia mizigo Bandarini. Mwisho
Serikali kupitia Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) imejipanga kujenga matenki ya kuhifadhi mafuta (Farm tanks) yenye uwezo wa kuhifadhi tani 360,000 kwa wakati mmoja. Ujenzi wa matenki hayo ni mpango mkakati wa kuwezesha meli zinazokuja kupakua mafuta zisikae Bandarini muda mrefu na hivyo kuongeza ufanisi na kupunguza gharama za ununuzi wa mafuta kwa mtumiaji wa mwisho. Maendeleo hayo yalibainika wakati Naibu Waziri wa Uchukuzi, Mhe. David Kihenzile alipofanya ziara yake ya kwanza ya kikazi katika Bandari ya Dar-es-Salaam tangia kuteuliwa kwake kama Naibu Waziri wa Wizara ya Uchukuzi. Katika ziara yake, Mhe. Kihenzile ametembelea eneo litakalojengwa matenki hayo ya kuhifadhi mafuta, eneo la kuhifadhi mizigo inayoharibika (perishable goods), gati la Mafuta la Kurasini Oil Jetty (KOJ), Gati Na. 1-7, Gati la Magari RoRo na Gati la Meli za kwenda Zanzibar na Visiwa vya Comoro. Baada ya ziara hiyo, Mhe. Naibu Waziri ameipongeza Menejimenti ya TPA na kuitaka kusimamia miradi hiyo ya kimkakati kikamilifu ili ikamilike kwa wakati na kuhakikisha thamani ya uwekezaji (value for money) inapatikana. Mwisho
Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Madini, Mhe. Dkt. Doto Biteko ametembelea Banda la Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) wakati wa kongamano la pili la wiki ya kitaifa ya Ufuatiliaji, Tathmini na kujifunza lililofanyika mjini Arusha. Katika kongamano hilo ambalo lilienda samba samba na maonyesho kutoka taasisi za umma zilizopewa fursa ya kuonyesha na kuelezea shughuli zao mbalimbali liliandaliwa na Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu. Pichani ni Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Mhe. Dkt. Doto Biteko akipewa maelezo kuhusu shughuli mbalimbali za Mamlaka na Afisa Mwandamizi wa Habari na Mawasiiano wa TPA, Bw. Leonard Magomba.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi Prof. Godius Kahyarara atembelea Banda la Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzana (TPA) wakati wa maonesho ya sita ya teknolojia ya Madini yaliyofanyika katika viwanja vya EPZA Bombambili Mjini Geita.
The Tanzania Ports Authority (TPA) has shone in the 18th East African trade fair held in Mwanza recently after winning the overall winner award. Besides the overall winning, TPA also emerged as the first winner for Central and Local Government Institutions, Departments and Agencies, Government Services/Agency Institutions and the first winner in the category of Best Exhibitor for Tanzania. , ,

Subcategories