The Tanzania Ports Authority (TPA) has shone in the 18th East African trade fair held in Mwanza recently after winning the overall winner award. Besides the overall winning, TPA also emerged as the first winner for Central and Local Government Institutions, Departments and Agencies, Government Services/Agency Institutions and the first winner in the category of Best Exhibitor for Tanzania. , ,
Bandari ya Tanga ipo katika hatua za mwisho kuandaa mchakato wa ujenzi wa magati meingine mawili mapya kwa ajili ya makasha na abiria. Akizungumza wakati wa ziara ya kutembelea na kukagua eneo litakaljengwa magati hayo mawili mapya, Naibu Mkurugenzi Mkuu, Mhandisi Juma Kijavara amesema mradi huo upo katika hatua za awali. “Magati hayo mawaili ni pamoja na gati la kwa ajili ya kuhudumia shehena ya makasha na gati kwa ajili ya kuhudumia abiria,” Mhandisi Kijavara. Mhandisi Kijavara amesema kwa sasa mradi huo upo katika hatua za awali za maandalizi ya kutangaza tenda katika mwaka wa fedha 2023/ 2024. Pamoja na kujipanga kwa mradi huu mkubwa, tayari Bandari hiyo imeshakamilisha maboresho ya miundombinu yake haswa ujenzi wa uboreshwaji wa magati, kuongeza kina na lango la kuingilia meli. Mradi huo, ulilenga kuongeza uwezo wa Bandari hiyo na kuboresha zaidi ufanisi wa utendaji wake katika kuhudumia wateja. Mwisho
Meli kubwa ya Makasha ya Mv Nordic Bc Munich imetia nanga katika gati jipya la Bandri ya Tanga. Hii ni mara ya kwanza kwa meli yenye urefu wa mita 180 na kina cha mita 7.4 kutoka nchini India kutia nanga katika bandari hiyo. Ujio wa meli kubwa kama hizi, ni matokeo ya maboresho ya mradi mkubwa wa Bandari ya Tanga, kwa sasa Bandari hiyo ina uwezo wa kuhudumia meli kubwa gatini, amesema Meneja Bandari ya Tanga, Mrisha Mrisha. Meli hiyo imebeba shehena ya mabomba kwa ajili ya mradi mkubwa wa maji katika Mkoa Tanga. Mradi huo una lengo la kutoa maji kutoka Mto Pangani kwenda katika miji ya Pangani, Muheza, Korogwe na Handeni. Mwisho
Na Mwandishi Wetu Serikali imeipongeza Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) kwa kutekeleza kwa ufanisi mradi wa upanuzi na maboresho ya Bandari ya Tanga ambao umefikia asilimia 99.5. Akizungumza bandarini hapo wakati wa ziara yake kukagua mradi wa maboresho wa bandari hiyo, Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kasim Majaliwa amesema maboresho hayo yalikuwa na tija sababu bandari hiyo imekaa kimkakati zaidi. “Bandari hii imekaa kimkakati zaidi kutokana na kutoa huduma nchini na nchi jirani kama vile DR Congo na Burundi,” amesema. DR Congo ndio soko kubwa kwa bidhaa zinazopita katika Bandari za Tanzania. Mradi wa maboresho wa Bandari ya Tanga ambao mpaka sasa umefikia asilimia 99.85%, umelenga kuongeza uwezo wa bandari hiyo na kuboresha Zaidi ufanisi katika kuhudumia wateja. Mbali na kuipongeza TPA, pia amewataka wafanyakazi wa Bandari ya Tanga kuongeza juhudi katika kazi zao ili wateja wanaotumia Bandari hiyo waendelee kuamini kuwa Bandari ya Tanga ni yenye ufanisi na mahali salama kwa mizigo hao. Katika hatua nyingine Waziri Mkuu, ameendelea kusisitiza kuwa kama Serikali itaendelea kuzipa nafasi Sekta binafsi kutoa huduma katika bandari ili huduma za utoaji mizigo ziweze kuharakishwa ikiwemo meli kukaa muda mfupi bandarini. Mwisho
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Burundi, Mhe.Gervais Ndirakobuca amesema ufanisi wa Bandari ya Dar es Salaam ndio uliosaidia kwa kiasi kikubwa kukua kwa uchumi wa nchi hiyo. Mhe. Ndirakobisca amesema hayo alipotembelea Bandari ya Dar es Salaam kwa lengo la kujifunza utendaji kazi wa bandari hiyo, Pamoja na kujionea maboresho makubwa ya miundombinu yaliyofanyika bandarini hapo. Ikumbukwe Bandari ya Dar es Salaam ilifanya maboresho makubwa ya miundombinu yake ikiwemo ujenzi wa magati yake kuanzia RoRo hadi gati namba 7. Mbali ya magati hayo, Bandari hiyo pia ilifanikiwa kuongeza kina cha maji magatini hadi kufikia urefu wa mita 14.5 na kuongeza kina cha sehemu ya kugeuzia meli na lango la kuingia bandarini. “Tumefurahishwa sana na kazi inafanyika hapa bandarini, na pia tunapongeza jitihada kubwa zinazofanywa na Serikali ya Awamu ya Sita katika kuboresha miundombinu ya Bandari hii muhimu kwetu” amesema. Amesema kwamba, kimsingi Bandari hii imesaidia sana kukuza uchumi wa nchi yetu ya Burundi. tunaomba MUNGU aendelee kuimarisha ushirikiano mwema uliopo kati ya Burundi na Tanzania. Aidha Waziri Mkuu Ndirakobuca ameishukuru Serikali ya Tanzania kwa jitihada zake za kuendelea kuboresha ulinzi katika mipaka ya Tanzania na Burundi na hivyo kuleta utulivu, kupunguza uharifu na kuwezesha shughuli za kiuchumi kufanyika. Wakitoa maelezo ya awali kuhusu utendaji kazi wa Bandari ya Dar es Salaam, Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi wa Tanzania, Mhe Prof. Makame Mbarawa pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa TPA, Bw. Plasduce Mbossa walimhakikishia Waziri Mkuu huyo kuwa Serikali itaendelea kufanya maboresho makubwa ya miundombinu katika Bandari zake ili kuongeza ufanisi. Mwisho
Jumla ya tani 20,000 za madini ya Shaba kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DCR) zinatarajiwa kusafirishwa kupitia Bandari ya Tanga kila mwezi. Kampuni kubwa ya uchimbaji Madini ya Shaba ya Cleancore kutoka (DCR) inatarajia kuanza kusafirisha sehena ya madini hayo kupitia bandari hiyo miezi michache ijayo. Hayo yalijulikana jana wakati wa ujumbe wa Kampuni hiyo uliongozwa na Mwenyeji wao ambaye ni Mwenyekiti wa Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania, Bi. Anjelina Ngalula.ulipotembelea Bandari ya Tanga ili kujionea maboresho makubwa yaliyofanywa na serikali. Mwisho
Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) imejipanga kuhudumia shehena ya mafuta ghafi kutoka Hoima nchini Uganda pindi uzalishaji wa bidhaa hiyo utakapoanza rasmi mwaka 2025. Tanzania ilishinda tenda ya kupitisha mafuta ghafi kwa njia ya bomba kutoka mji wa Hoima yanapozalishwa hadi kwenye masoko ya nje kupitia Bandari ya Chongoleani mjni Tanga . Uamuzi wa Mwisho wa Uwekezaji wa miradi ya juu na EACOP ulitangazwa tarehe 1 Februari, 2022 na maendeleo ya mradi yanaendelea kwa lengo la Mafuta ya Kwanza mwaka 2025. Haya yalisemwa hivi karibuni na Mkurugenzi wa Masoko na Uhusiano, Dkt. George Fasha wakati wa mkutano na maonyesho ya 10 wa Mafuta ya Afika Mashariki uliofanyika Nchini Uganda. Dkt Fasha ambaye alikuwa ni mmoja wa wasilishaji mada katika mkutano huo, alisema TPA kupitia Bandari yake ya Chongoleani iliyopo mjini Tanga, imejipanga kuhudumia shehena hiyo kwa ufanisi mkubwa. Amesema kwamba Bandari ni Lango la Biashara, Kitaifa na Kimataifa, hivyo kama ikitumiwa ipasanvyo itafungua milango ya biashara na maendeleo ya kiuchumi kwa nchi za Afrika Mashariki. “Ili kufanikisha haya, tuna mradi mkubwa wa kimkakati unaojulikana kama DMGP ambao umejikita katika kufanya maboresho ya kimiundombinu kwa Bandari ya Dar es Salaam,” alisema Dkt. Fasha. Mradi huu unahusisha pamoja na mambo mengine, maboresho ya kiutendaji kwa wafanyakazi wetu ambao wamepatiwa mafunzo mablimbali ya jinsi ya kuhudumia meli na mizigo inayopita Bandari ya Dar es Salaam na zinginezo. Mkutano huo uliolenga kuionyesha Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) kama kimbilio la chaguo la fursa za uwekezaji wa mafuta na gesi ili kuboresha mageuzi ya kijamii na kiuchumi. Bandari ni lango la biashara na kama ikitumiwa ipasanvyo itafungua mialngo la biashara na maendeleo ya kiuchumi. Ili kufanikisha haya, tuna mradi mkubwa wa kimkakati ujulikano kama DMGP ambao lengo lake ni kufanye maboresho ya kimiundombinu kwa Bandari ya DSM Mradi huu unahusisha Pamoja na mambo mengine pia na maboreho ya kiutendaji wa wafanyakazi wetu ambapo wamewezeshwa kwa kupata mafunzo mablimbali ya jinsi ya kuhdumia meli na mzigo inayopita Bandarini. Mwisho

Subcategories